Mazungumuzo Ya UASU Na Serikali
1st August, 2012
Vyama vya kutetea masilahi ya wafanyikazi wa Vyuo Vikuu vya kitaifa vimeilaumu Serikali kwa kuchelewesha makusudi mazungumzo ya kutekeleza nyongeza ya mishahara na marupurupu yao. Waziri wa Elimu ya Juu Prof. Margaret Kamar hata hivyo hii leo ameanzisha rasmi mazungumzo hayo, huku akikumbana na wakati mgumu kutoka kwa viongozi wa Kitaifa wanaowawakilisha wafanyikazi hao wanaowalaumu manaibu wakuu wa vyuo vikuu kwa kupuuza haki za wafanyikazi. Frank Otieno na taarifa hiyo.