Moi awataka viongozi kueneza amani
28th July, 2012
Rais mstaafu Daniel Toroitich arap Moi sasa anawataka viongozi wote nchini kujenga taifa hili bila kuzingatia misingi ya kikabila na pia kusisitiza amani. Alisema kwamba baadhi ya viongozi wanaotembea kote nchini katika ziara zao za mikutano hawazungumzii swala la amani na pia hawajaonyesha ishara za kufanya hivyo huku idadi kuu wakiwa hawana nia yeyote ya kutimiza hatua hio ya amani baina ya wananchi kwote nchini.