Vilabu vya pombe vyafungwa Nyeri
17th July, 2012
Katika habari ambazo ni pigo kubwa kwa wanywaji wa vileo katika mkoa wa kati na kwa wafanyibiashara wa sekta hii,vilabu kadhaa vimefungwa eneo hilo kutokana na kile kinachotajwa kuwa ukiukaji wa sheria ya mahakama inayotoa idhini ya uuzaji wa pombe. Kwa mfano katika wilaya ya nyeri kusini vilabu sita tayari vimefungwa na nyeri ya kati vilabu zaid ya arobaine. Wenyewe hata hivyo wataruhusiwa kuuza pombe waliosalia nayo kwa miezi mitatu ijayo pekee yake. Ni hatua ambayo bila shaka itapokewa kwa mseto wa hisia kutoka kwa wateja na wafanyibiashara. Carol Nderi na taarifa kamili.