.
22nd June, 2021
Ni afueni kwa taifa na kwa wale ambao walikuwa wanasubiri kupokea chanjo yao ya pili dhidi ya virusi vya korona baada ya Kenya kupokea msaada wa dozi 358,700 za chanjo dhidi ya virusi vya covid?19 kutoka nchini Denmark. Kuwasili kwa chanjo hiyo kunatarajiwa kupiga jeki awamu ya pili ya utoaji wa chanjo nchini na huku serikali ikijizatiti kuanzisha shughli ya usambazaji wa chanjo hizo, swala ibuka ni iwapo chanjo hizo zitatumika zote kabla ya muda wa mwisho wa kutumika kufika.