×
The Standard Group Plc is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services. The Standard Group is recognized as a leading multi-media house in Kenya with a key influence in matters of national and international interest.
  • Standard Group Plc HQ Office,
  • The Standard Group Center,Mombasa Road.
  • P.O Box 30080-00100,Nairobi, Kenya.
  • Telephone number: 0203222111, 0719012111
  • Email: [email protected]
Premium

Bei ya petroli ya ongezeka

News

Wakenya wanatarajiwa kuendelea kugharamika zaidi kununua mafuta baada ya bidhaa hiyo kupanda katika tangazo la hivi karibuni la Mamlaka ya Kutathmini Bei ya Kawi ERPA.

Katika bei hiyo ambayo itatumika kwa mwezi mmoja ujao, bei ya petroli imepanda kwa shilingi 3 na senti 40 huku ile ya dizeli ikipanda kwa shilingi sita na senti 40.  Bei ya mafuta taa imepanda kwa kiwango cha juu zaidi kwa shilingi 15 na senti 19. Bei hii mpya sasa inafikisha bei ya petroli jijini Nairobi kuwa shilini 182.70  huku ile ya dizeli ikifika shilingi 161.13.

Bei hii imepanda licha ya mpango mpya wa hivi karibuni ambapo serikali iliwekwa mkataba wa kununua mafuta hayo kwa deni na wauzaji nchini Kenya wakiruhusiwa kuyalipa kutumia shilingi ya Kenya.

Wiki iliyopita Waziri wa Kawi Davis Chirchir alitaja mpango huo unaendelea vyema, jinsi tu ilivyopangwa.

Haya yanajiri huku bei hiyo ikitarajiwa kupanda hata zaidi iwapo mapendekezo ya katika Mswada wa Kifedha yatapitishwa. Mapendekezo hayo yanarejesha Kodi ya Thamani ya Ziada kwa bidhaa za mafuta kuwa asilimia 16 baada ya kuwa asilimia 8 katika bajeti iliyopita.

Hata hivyo, Rais William Ruto ametetea hatua hii akisema inalenga kusawazisha viwango vya kodi na kuzuia ulaghai. Kadhalika ameongeza kwamba ili kuhakikisha kwamba bei haipandi sana amepunguza kodi nyingine mbili ambazo jumla yake ni asilimia 5.

Related Topics


.

Trending Now

.

Popular this week