Kitendawili kinazidi kuuzingria uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ICC wa kutoa hati ya kukamatwa kwa Rais wa Urusi Vladmir Putin.
Katika hati hiyo, ICC imemtuhumu Putin kuhusika katika uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kuwahamisha watoto kutoka Ukraine kwenda Urusi kinyume na sheria.