Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis leo Jumamosi atakutana na waathiriwa wa vita vya wenyewe kwa wenyewe na viongozi wa kidini nchini Sudan Kusini katika siku ya pili ya ziara yake kwenye taifa hilo linalokabiliwa na machafuko.
Mkutano huo unafuatia wito alioutoa Papa Francis siku ya Ijumaa kwa viongozi wa Sudan Kusini akiwataka kutafuta amani ya kudumu na kukomesha mateso yanayowakumba raia.