Mnamo Jumanne wiki hii nikiwa mtaa wa Mwiki, eneo la Kasarani, nilishuhudia kisa ambacho kingali kunipiga moyo hadi sasa.
Nilikuwa nimekwenda eneo hilo kuwanasa wanafunzi na walimu wao kuhusu maandalizi ya mitihani ya taifa.
Aidha, nilitaka pia kujua ni kwa vipi walivyo na imani na timu mpya iliyochukua uongozi wa Baraza la Taifa la Mitihani Nchini kutokana na uozo wa wizi wa mitihani mwaka jana ulijitokeza katika afisi iliyokuwepo KNEC.