Leo hii kama kweli baraza la wazee wa jamii ya Wakamba wangelitambua dosari lililosababishwa na gavana wa Machakos, Alfred Mutua kwa wanaume chungu nzima wa Kenya na barani Afrika, yamkini wangeitisha kikao cha dharura kumpa kisomo gavana huyu.
Kisomo cha kwanza ni kumuonya wazi kwamba ni mtoto peke yake ambaye anaweza kulalamika kunyanyaswa na mtoto mwenzake lakini siyo jibaba lenye cheo cha ugavana kama yeye, kulalamikia juu ya mwanaume ama wanaume wenzake.