Yalianza kama makundi yenye misimamo kinzani ya kisiasa nchini, lakini kadri muda ulivyosonga, siku zika pita, Kieleweke na Tanga Tanga yakaibukia kuwa makundi mawili ya kisiasa tajika yaliyo kita mizizi katika ulingo wa kisiasa huku kila upande ukijitahidi kunadi sera zake ili kuwashawishi wananchi kuwaunga mkono.
Mwaka uliopita baada Rais Uhuru Kenyatta na aliye kuwa waziri mkuu Raila Odinga kukubaliana kufanya kazi kwa pamoja maarufu kama ‘Handisheki’ mirengo miwili ya kisiasa ikabuniwa.