Huku maafi sa wa idara za EACC na DCI zikiwazamia mameneja wakuu wa halmashauri ya bandari nchini, KPA, mengi yazidi kujitokeza kwamba huu ni mtego wa abunuwasi utakaowanasa waliomo na hata wale wasiokuwemo.
Bandari hii ya KPA, imegeuzwa kuwa uwanja wa fujo, karaha, unyanyasaji, utapeli, kisiwa cha giningi na kitega uchumi kwa wanasiasa wakubwa wanaosimamia makundi yote mawili ya “Handisheki” na “Tanga Tanga”.