×
App Icon
The Standard e-Paper
Read Offline Anywhere
★★★★ - on Play Store
Download Now

Uwanja wa shule wageuzwa soko la dawa za kulevya Mombasa

Picha ya wanaotumia dawa ya kulevya. [Picha: Pambazuko]

Uwanja wa shule ya Msingi ya Freea town umegeuzwa sasa kuwa uwanja wa kuuza dawa za kulevya hasa katika siku za wikendi. Kila siku za Jumamosi na Jumapili uwanja huo hujaa mamia ya watu wengi wao wakitazama mpira huku wengine wakifanya biashara ya kukodisha viti kwa watu ambao wamekuja kutizama mpira,ambao huwa unachezwa hasa kila wikendi katika uwanja huo.

Katika siku hizo ni nadra sana kuona maafisa wa polisi wakizunguka ili kuangalia hali ya usalama iko namna gani, ikizingatiza kuwa kuna idadi kubwa ya watu ambao usalama ungehitajika kwa maana huenda hata zogo likatokea katika uwanja huo. Katika siku hizo za wikeendi pia mimi huenda katika uwanja huo ili kutazima mpira lakini cha kushangaza huwa ninatazama “mpira tafauti,” nilipata mahali nikasimama na kuegemea ukuta wa shule ya Freea Town, ili nipate fursa ya kuuangalia mpira vizuri. Hata hivyo kando yangu kulikuwa na vijana ambao hata wengine walikuwa wamelala na wengine wakiuza bangi na dawa nyengine za kulevya kisiri.

Get Full Access for Ksh299/Week
Unlock the Full Story — Join Thousands of Informed Kenyans Today
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in