Uwanja wa shule ya Msingi ya Freea town umegeuzwa sasa kuwa uwanja wa kuuza dawa za kulevya hasa katika siku za wikendi. Kila siku za Jumamosi na Jumapili uwanja huo hujaa mamia ya watu wengi wao wakitazama mpira huku wengine wakifanya biashara ya kukodisha viti kwa watu ambao wamekuja kutizama mpira,ambao huwa unachezwa hasa kila wikendi katika uwanja huo.
Katika siku hizo ni nadra sana kuona maafisa wa polisi wakizunguka ili kuangalia hali ya usalama iko namna gani, ikizingatiza kuwa kuna idadi kubwa ya watu ambao usalama ungehitajika kwa maana huenda hata zogo likatokea katika uwanja huo. Katika siku hizo za wikeendi pia mimi huenda katika uwanja huo ili kutazima mpira lakini cha kushangaza huwa ninatazama “mpira tafauti,” nilipata mahali nikasimama na kuegemea ukuta wa shule ya Freea Town, ili nipate fursa ya kuuangalia mpira vizuri. Hata hivyo kando yangu kulikuwa na vijana ambao hata wengine walikuwa wamelala na wengine wakiuza bangi na dawa nyengine za kulevya kisiri.