Wengi juzi walishangaa na kupigwa na butwaa kuwaona wanasiasa wawili mashuhuri wa pwani, Gavana wa Mombasa Hassan Ali Joho na mbunge wa Malindi anayeng’ong’ongwa na chama cha ODM Aisha Jumwa wakikumbatiana kama pwagu na pwaguzi mjini Malindi wakiduwaa kama kweli kunao uhasama wa kisiasa baina yao.
Wafuasi wa pande zote mbili, wanaoshinikiza Jumwa kusukumwa pembeni na wale wanamtetea kwamba anaonewa na chama hawafahamu kwamba wanasiasa wote ni sungura wajanja wakitegemea msemo mmoja kwamba katika siasa hamna hadui ama rafiki wa kudumu.