Gavana Mruttu amewashauri wakulima wenye mashamba yanayonyunyiziwa maji kuuza mazoa yao katika msimu huu kufuatia njaa inayolikumba taifa la Kenya.
Akizungumza na wakulima wa Majengo/Marodo katika wadi ya Mboghoni Taveta, gavana Mruttu alisema kuwa hii ndio nafasi ya kipekee kwa wakulima hawa kufaidika kutokana na bidii yao katika ukulima kufuatia mhemuko wa bei ya vyakula sokoni.