Je, ni nani anayesema ukweli hapa? Je, ni nani wa kusingiziwa hapa? Je, ni yupi aliyetoa ahadi za uongo jukwaani? Haya ni baadhi ya maswali ambayo Wakenya wengi wanazidi kujiuliza.
Hatua aliyoichukuwa kiongozi wa walio wengi bungeni Aden Duale kudinda kutoa orodha ya wafadhili wa ugaidi ni pigo kuu kwa waliopoteza wapendwa wao katika mashambulizi ya kigaidi. Tukio hili limewaacha wengi vinywa wazi baada ya Duale kubadili msimamo wake wa awali.