Shirika la msalaba mwekundu limeripoti kuwa zaidi ya watu 15 wamefariki na wengine 75,000 wamepoteza makao yao na kulazimika kuwa wakimbizi wa ndani kwa ndani baada ya kuathirika pakubwa na mafuriko yaliyoathiri sehemu nyingi humu nchini. Familia nyingi zimepoteza rasili mali zao huku ikihofiwa kuwa endapo suluhu ya kudumu haitapatikani basi, maafa ya mafuriko yatazidi kuathiri wengi miaka nenda miaka rudi.