Maafisa wa polisi wa Machakos mjini wamemkamata mwanaume mmoja ambaye amemjeruhi mwenzake wa umri wa makamo kwa kummwagilia asidi kwenye sehemu zake za siri kufuatia tofauti baina yao walipokuwa wakivinjari, katika soko la Kathome lililo kijiji cha Kalama, Kaunti ya Machakos.
Mwanamume huyo anaendelea kutibiwa katika hospitali ya Machakos level 5 anaeleza alikuwa katika baa moja akiwa na wenzake na wakati wa kuondoka ndipo mvutano ukaanza kisha mshukiwa akamwangusha na akammwagilia asidi hiyo.
Kamanda wa Polisi wa Machakos mjini Joseph Tenai amesema mshukiwa anaendelea kuzuiliwa katika kituo cha polisi cha Machakos huku uchunguzi ukiendelea.