Watu wawili wakamatwa na Misokoto ya bangi Shanzu

Maafisa wa Polisi wanawazulia watu wawili waliokamatwa katika Eneo la Shanzu Kaunti ya Mombasa wakiwa na misokoto ya bangi. Kamanda wa Polisi kwenye kaunti hiyo, Johnson Ipara amesema wawili hao walikamatwa kwenye msako ulioendeshwa katika eneo hilo mapema leo kuwanasa walangunzi na wafanyabiashara wa dawa za kulevya.

Amesema wawili hao Cynthia Achieng na Frederick Ogutu walikuwa wameisafirisha misokoto hiyo yenye thamani ya shilingi elfu 682, 000 kutoka Kaunti ya Migori na walikuwa wanalenga kuiuza kwenye Kaunti za Mombasa, Kilifi na Kwale.

Ipara aidha ameonya kwamba polisi hawatalegeza kamba dhidi ya walanguzi wa mihadarati. Amesema biashara zote haramu zitakabiliwa kwa mujibu wa sheria.

Amedokeza kwamba mwaka jana, Cynthia alikabiliwa na mashtaka ya ulanguzi wa dawa za kulevya japo akaachiliwa kwa dhamana.

Wawili hao ambao wanazuiliwa katika Kituo cha Polisi cha Central jijini Mombasa, wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho ili kufunguliwa mashtaka

Related Topics