Mahakama jijini Nairobi imetupilia mbali ombi la aliyekuwa Gavana wa kaunti ya Nairobi, Evans Kidero kutaka kesi zinazomkabili kutojumuishwa wakati wa kusikilizwa.
Jaji Douglas Ogot ametupilia mbali ombi hilo akisema upande wa mshtakiwa haujatoa sababu mwafaka kuishawishi mahakama kukubali ombi lenyewe.