Jaji wa Mahakama ya Juu, Njoki Ndung'u ameiandikia Idara ya Upelelezi, DCI akiitaka kuanzisha uchunguzi dhidi yake na majaji wengine katika mahakama hiyo kufuatia madai ya ufisadi.
Kwenye barua hiyo, Jaji Ndung'u amesema madai yanayoibuliwa ni yenye uzito na yanapaswa kuchunguzwa ili kubaini ukweli.