Naibu wa Rais, William Ruto amezitaja kuwa ufisadi, siasa zinazoendelezwa kwa misingi ya kukabili jinamizi hili. Akihutubu wakati wa halfa moja kwenye Kaunti ya Mombasa, Ruto amesema licha ya serikali kuwekeza kwa idara zilizojukumiwa kukabili ufisadi, kuna watu walio na njama fiche ambao wanalenga kuzitumia idara hizo kwa manufaa binafsi.
Siku chache zilizopita Ruto alimshtumu Mkurugenzi wa Idara ya Upelelezi, DCI George Kinoti kwa madai ya kutumiwa kisiasa katika njama ya kutatiza miradi ya maendeleo ya serikali kwa kisingizio cha kukabili ufisadi japo Kinoti amesisitiza kuwa ofisi yake haitatishwa na yeyote katika kutekeleza majukumu yake.