Mwanaharakati Caroline Mwatha alifariki baada ya kutokwa damu kupita kiasi alipojaribu kuavya mimba. Daktari Peter Muriuki Ndegwa aliyeiwakilisha familia yake, amesema marehemu Caoline alikuwa na ujauzito wa kati ya miezi mitano na sita. Upasuaji uliofanyiwa mwili wake katika Hifadhi ya Maiti ya Umash , Nairobi umethibitisha hilo na kubainisha kuwa kijusi cha kiume kilikuwa bado kwenye uterasi. Pia uterasi wenyewe uliharibiwa vibaya, na kusababisha damu nyingi kuingia kwenye tumbo. Aidha mpasuaji huyo alisema kichwa cha kijusi hicho kilikuwa kimejeruhiwa kidogo, na mwili wake ulikuwa rangi ya kijivu, ishara ya kupoteza damu nyingi.
Wakati uo huo, dakatari Ndegwa amesema Marehemu hakuwa na majeraha yoyote ila yale ya sindano hivyo kufutilia mbali madai kuwa huenda alidhulumiwa kabla ya kifo chake. Ndegwa alisema uchunguzi zaidi utafanywa ili kubaini dawa iliyotumika kufanikisha shughuli hiyo.