Rais asutwa na Raila

Na, Beatrice Maganga
Rais asutwa na Raila
Baada ya kinara wa NASA, Raila Odinga kuhudhuria hafla moja na Rais Uhuru Kenyatta katika Kaunti ya Kiambu na kuonesha kuwa tayari kukubali matokeo ya marudio ya uchaguzi wa urais,  ametoa taarifa nyingine kumshtumu Rais kwa madai ya kupanga kusalia mamlakani kiimla.
Akizunguzma katika kikao na wanahabari,  Raila amesema tangu Mahakama ya Juu ilipotoa uamuzi wake, hajazungumzia dosari zilisohuhudiwa wala kuikemea IEBC kwa kuendesha uchaguzi usioridhisha na badala yake kuendelea kuwakashifu majaji.
Kadhalika ameweka wazi kwamba iwapo Rais Kenyatta hataonesha heshima kwa idara ya mahakama, huenda Wakenya wakalazimika kutafuta mbinu za kuhakikisha anaiheshimu katiba.

Related Topics