Uchumi na Biashara Podcast; Usidharau Mutura, inanipa mapato tosha
Uchumi na Biashara
Jan. 20, 2022
Mutura ni mojawapo ya kitoweo kinachopendwa na wengi, mutura huuzwa nyakati za jioni jioni, wateja wakisema utamu wake ni giza, vumbi na kutojua unakula nyama ya nini hasa. Mutura ni mchanganyiko wa vipande vipande vya nyama, wenyewe huita sausage ya watu wa kawaida. Caleb Kimtai, mfanyabiashara mjini Makutano Kaunti ya Pokot Magharibi amezungumza na mwanahabari wetu Moses Kiraese na anakiri kuwa japo baadhi hudharau mutura, anajua siri ni nini kwani kupitia mutura, anakimu familia yake na pia ametekeleza miradi mbalimbali nyumbani kwao
RELATED EPISODES
Mbona Magari ya Umeme? | Uchumi na Biashara Podcast
Kuvuma kwa Utalii Krisimasi na Mwaka Mpya | Uchumi na Biashara Podcast
Serikali saidia, biashara zetu zazorota | Uchumi na Biashara Podcast