Serikali saidia, biashara zetu zazorota | Uchumi na Biashara Podcast
Uchumi na Biashara
Oct. 29, 2022
Licha ya serkali kuahidi kushughulikia changamoto za wafanyabiashara wadogo wadogo, bado mahangaiko yanashuhudiwa mwezi mmoja baada ya Kenya Kwanza kuchukua hatamu za uongozi. Wengi wa wafanyabiashara hao wanalalamikia kuongezwa kwa bei ya mafuta, na kusababisha hasara katika sekta ya matatu. Charles Macharia, mhudumu wa teksi na Jimmy Mwangi, mhudumu wa matatu wanatishia kugura biashara hii. Mwanahabari wetu Edwin Mbugua amefanya mazungumzo na baadhi ya wafanyabiashara hao katika Kaunti ya Nyeri.
RELATED EPISODES
Mbona Magari ya Umeme? | Uchumi na Biashara Podcast
Kuvuma kwa Utalii Krisimasi na Mwaka Mpya | Uchumi na Biashara Podcast