×
App Icon
The Standard e-Paper
Informed Minds Prefer The Standard
★★★★ - on Play Store
Download Now

Mudavadi: Wakenya 400 watapeliwa kazi ughaibuni

Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi akikutana na maafisa wa ngazi za juu wa maswala ya mambo ya nje. [Kwa hisani ya X]

Kenya imepiga kengele ya tahadhari kuhusu kuongezeka kwa visa vya usafirishaji haramu wa raia wake kuelekea Asia ya Kusini Mashariki, ikilitaja eneo hilo kama tishio ambako watu wanaotafuta ajira wanadanganywa na kuishia katika mitandao ya ulaghai wa mtandaoni na ajira za kulazimishwa.

Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi, Mkuu wa Mawaziri Musalia Mudavadi ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Nje, alisema takribani Wakenya 400 wamekumbwa na mtego huo wa mawakala wa uajiri wasio waaminifu wanaotoa ahadi za kazi zenye malipo makubwa nchini Vietnam, Urusi, Cambodia na Myanmar, lakini mwishowe hujikuta katika hali aliyoielezea kama “aina ya utumwa wa kisasa.”

Get Full Access for Ksh299/Week
Uncover the stories others won’t tell. Subscribe now for exclusive access
  • Unlimited access to all premium content
  • Uninterrupted ad-free browsing experience
  • Mobile-optimized reading experience
  • Weekly Newsletters
  • MPesa, Airtel Money and Cards accepted
Already a subscriber? Log in