Rais William Ruto na mwenzake wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, wameahidi kushirikiana kuimarisha urafiki kati ya Kenya na Tanzania, kukiwamo kuondoa vikwazo vya kibiashara kwenye mipaka ya mataifa haya mawili.
Aidha, Rais Ruto amekariri kwamba ataendeleza ushirikiano uliowekwa na mtangulizi wake, Uhuru Kenyatta kwa manufaa ya raia wa nchi hizi mbili.