11th June, 2021
Ujenzi wa barabara inayounganisha karandi katika kaunti ya Laikipia na Marigat katika kaunti ya Baringo, utakamilika baada ya mwezi julai mwaka ujao. Mradi huo ambao umefanyika kwa asilimia 55 kwa sasa unagharamiwa na serikali kuu na unatarajiwa kuimarisha hali ya maisha ya wakazi wa Baringo kusini. Huyu hapa mwanahabari wetu Ibrahim Karanja na mengi kuhusu mradi huo wenye gharama ya shilingi bilioni tano.