5th June, 2020
Hii leo kwenye makala yetu ya kila ijumaa ya mirindimo tunaangazia sarakasi ndani ya chama cha Simba cha Ford Kenya ambapo viongozi wake wamekuwa wakioneshana ubabe wa nani mkali haswa kwenye wadhfa wa urathi wa chama hicho. Halikadhalika msimamo wa mbunge wa Ugenya David Ochieng umeonekana kumkeketa maini mwenyekiti wa chama cha ODM John Mbadi huku waziri Kagwe na Rais John Pombe Magufuli wakioenkana kukerwa na mambo fulani.