29th May, 2020
Waziri wa elimu, Profesa George Magoha, leo hii ameipokea ripoti kutoka kwa kamati aliyoiteua kuangazia athari za janga la korona kwa sekta ya elimu. Japo Magoha amefafanua kwamba mapendekezo kwenye ripoti hiyo ni kauli na hoja kutoka kwa wadau mbalimbali, amekariri kwamba ufunguzi wa shule utategemea zaidi ushauri wa madaktari na wataalam wa afya.