22nd May, 2020
Mwenyekiti wa baraza la taasisi ya mafunzo ya utabibu, KMTC, Prof Philip Kiloki amesema chuo hicho na vingine vyote nchini vitazidi kutoa misaada ya chakula kwa makundi yasiyobahatika katika jamii haswa wakatii huu wa janga la korona. Alisema hayo wakati wa kutoa chakula kwa makao ya watoto hapa Nairobi.