22nd May, 2020
Jamii ya waislamu wakiadhimisha ijumaa ya mwisho ya mwezi mtukufu wa Ramadhan baraza kuu la waislamu SUPKEM limewaonya jamii ya waislamu dhidi ya kuvunja maagizo ya kutokongamana yaliyowekwa na serikali kudhibiti kuenea kwa virusi vya homa ya korona. Mwenyekiti wa SUPKEM Hassan Ole Naado amewahimiza waislamu kuswali majumbani mwao wakati wa kusherehekea sikukuu ya IDD inayotarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi au Jumapili.