.
1st February, 2020
Wito wa utangamano wa kitaifa ulitawala hafla ya kutawazwa kwa askofu wa kanisa la katoliki Dominic Kimengich ambaye alitawazwa rasmi hii leo katika kanisa la seminari la mothers of apostles mjini Eldoret kaunti ya uasin gishu ambapo sasa atakuwa askofu mpya wa dayosisi ya Eldoret .Ni hafla iliyohudhuriwa na viongozi wa dini wakiongozwa na kadinali John Njue pamoja na wanasiasa akiwemo naibu wa rais William Ruto, seneta wa kaunti baringo Gideon Moi, magavana pamoja na wabunge .