31st January, 2020
Takriban wakaazi 250 wa mtaa wa Kiganjo mjini thika walitoroka makwao jana baad aya madai ya kuvamiwa na majambazi waliokodoshwa kuwafurusha katika ardhi iliyo na umiliki tata. Watu hao walifika usiku na kuzunguza ua katika ardhi ya Ekari 5 inayosemekana kuzozaniwa na wawekezaji wawili tofauti.aidha habari zinarifu kuwa shamba hilo linamilikiwa na marehemu Margret Wangui Kimani ila mmiliki mwengine chini ya kampuni ya Aberdare land owners wakajitokeza baada ya ardhi hiyo kugawanywa mwak wa 2013.