31st January, 2020
Hafla ya kumuapisha Naibu Gavana wa Kiambu Daktari James Nyoro inafanyika hii leo baada ya shughuli hiyo kusitishwa hapo jana kutokana na vikwazo vya kisheria. Nyoro anaapishwa kuchukua mahali pake Ferdinand Waititu ambaye Bunge la Seneti liliidhinisha kutimuliwa kwake kwenye kikao kilichoandaliwa siku ya Jumatano.