13th January, 2020
Mwanamume Mmoja Ametiwa Nguvuni Kwa Kumnajisi Msichana Mwenye Umri Wa Miaka 16 Wa Kidato Cha Pili Kijijini Yamo Kaunti Ndogo Ya Samburu Ya Kati. Inadaiwa Wakati Wa Kuokolewa Kwa Msichana Huyo, Alikuwa Na Mtoto Mdogo Mwenye Umri Wa Siku Mbili. Sasa Msichana Huyo Na Mwanawe Wako Mikononi Mwa Serikali Huku Chifu Domick Lempara Akisema Uchunguzi Ungali Unaendelea.