3rd January, 2020
Klabu Ya Sofapaka Imezindua Wachezaji Kumi Na Mmoja, Mkondo Wa Pili Wa Ligi Kuu Ya Taifa Kpl Ukitarajiwa Kung'oa Nanga Wikendi Hii. Rais Wa Sofapaka Elly Kalekwa, Kocha John Baraza Na Ajenti Wa Baadhi Ya Sajili Wapya Prince Koyi Kwa Pamoja Wamewasifia Wachezaji Hao Wakisema Wataisaidia Klabu Hiyo Katika Maazimio Yake. Miongoni Mwa Waliosajiliwa Ni Wachezaji Wanne Kutoka Mataifa Ya Cameroon, Ghana Na Uganda. Sofapaka Wanawaalika Kariobangi Sharks Jumamosi Hii Ugani Kenyatta Kaunti Ya Machakos.