Muthama amuonya Kalonzo kwa madai ya kumuunga Rais Uhuru Kenyattta
26th December, 2019
<style type="text/css">p.p1 {margin: 0.0px 0.0px 0.0px 0.0px; line-height: 20.1px; font: 10.0px Arial}
span.Apple-tab-span {white-space:pre}
</style>
Aliyekuwa seneta wa machakos Johnston Muthama amemuonya kingozi wa wiper kalonzo musyoka kuwa huenda akajipata akistaafu kisiasa pamoja na Rais Uhuru Kenyatta asiposikiza ushauri wa wanasiasa wenza kutoka eneo la ukambani. Muthama aliyasema haya saa chache kabla ya wandani wa Kalonzo kwenye chama cha wiper kujitokeza wakimtaka Muthama kujiuzulu kutoka kwa chama cha Wiper. Gavana wa machakos alfred mutua sasa ametangaza kuunga mkono matamshi ya Muthama.