16th December, 2019
Polisi Mjini Busia Wamenasa Gari Moja Lililokuwa Likisafirisha Zaidi Ya Misokoto 1,5oo Ya Bangi, Kisha Kuwakamata Washukiwa Watatu Katika Eneo La Road Block Kwenye Barabara Kuu Ya Busia?Kisumu. Kulingana Na Kamanda Wa Polisi Kaunti Ya Busia John Nyoike, Gari Hilo Aina Ya Toyota Limenaswa Na Maafisa Wa Polisi Waliokuwa Wakipiga Doria Katika Kizuizi Cha Polisi Mwendo Wa Saa Tano Asubuhi. Bangi Hiyo Inashukiwa Kusafirishwa Kutoka Nchi Jirani Washukiwa Hao Watatu Waliwekwa Korokoroni Na Watafikishwa Mahakamani Leo.