10th December, 2019
Wauguzi wapatao 1000 katika kaunti ya Kiambu na kaunti jirani wameanzisha kampeni ya kuwasilisha malalamishi kwa usimamizi wa uchukuzi wa reli ya kisasa ama SGR kuhakikisha treni zina wahudumu walio na mafunzo ya kutosha kutoa huduma za matibabu. kampeni hii ilianzishwa siku 5 zilizopita kufuatia kifo cha Florence kamene Muhia aliyefariki bada ya kudaiwa kukosa kupata huduma ya haraka ya matibabu alipokuwa safarini akiwa kwenye treni ya SGR kutoka Mombasa akija hapa nairobi . wakizungumza katika hospitali yaThika Level 5 wakati wa ibada ya wafu kwa mwendazake, jamaa na marafiki wa Florence walielezea namna juhudi zao za kumtafutia huduma za matibabu kutoka kwa usimamizi wa sgr ziligonga mwamba.