10th December, 2019
Shughuli za chukuzi wa umma katika eneo la Mbooni, kaunti ya Makueni zilitatizika baada ya madereva wa matatu, kuandamana wakidai kuwa wenzao walio na magari ya Probox wanawanyanganya biashara ya uchukuzi ilhali hawana kibali cha kuhuduma katika sekta hiyo. Wahudumu hao wa matatu ni wale hufanya uchukuzi katika barabara za Kikima kuelekea ?Tawa?Masii?Machakos hadi Nairobi na vile vile wengine wanaohudumu kuelekea Wote?Makindu na Kibwezi.
Eneo la Mbooni lina magari mengi ya Probox ambayo yanapatikana katika kila barabara huku madereva wakidaiwa kukiuka sheria za trafiki kwa kubeba watu wengi kupita kiasi hadi sehemu ya nyuma ya gari kinyume cha sheria. Mgomo huo uliwafanya abiria wengi wanaosafiri kwenda sehemu mbali mbali kutatizika huku wengi wao ambao walikuwa wakielekea maeneo ya karibu wakilazimika kutumia pikipiki.