10th December, 2019
Gavana wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko amelazwa katika hospitali ya kitaifa ya kenyatta baada ya kuugua usiku wa kuamia leo akiwa katika gereza la kamiti.hapo jana hakimu mkuu wa mahakama ya milimani douglas ogoti alimruhusu sonko kutafuta matibabu. Sonko pamoja na washukiwa wengine walikanusha mashtaka ya ufisadi dhidi yao na wataendelea kuzuiliwa hadi hapo kesho kesi ya kutaka kupewa dhamana itakapoamuliwa. Mawakili wa sonko walitaka mteja wao kupewa dhamana kwa msingi kwamba ni mgonjwa na atahitaji matibabu. Hata hivyo upande wa mashtaka ulikataa ombi la sonko kwa msingi kwamba huenda akahepa.