9th December, 2019
Mbunge wa Nyeri mjini Wambugu Ngunjiri sasa amewanyoshea kidole cha lawama maafisa wa polisi akiwalaumu kwa kile ametaja kuwa utepetevu kufuatia vurumai zilizoshuhudiwa Nyeri hapo jana kwenye hafla ya kuchangisha fedha iliyohudhuriwa na naibu rais William Ruto katika shule ya upili ya wavulana ya giakanja. Vurugu hiyo inasemekana kuwahusisha wakazi wanaoaminika kuwa wafuasi wa mbunge huyo waliokuwa wakikabiliana na kundi jingine likiaminika kuwa la wafuasi wa naibu wa rais.