6th December, 2019
Gavana Wa Nairobi Mike Mbuvi Sonko Amekamatwa Na Kuhojiwa Kwa Saa Kadhaa Katika Tume Ya Kupmabana Na Ufisadi. Sonko Alikamatwa Huko Voi Saa Chache Baada Ya Mkurugenzi Mkuu Wamashtaka Noordin Haji Kutoa Agizo La Kukamatwa Kwake. Kulizuka Kizaazaa Wakati Wa Kukamatwa Kwake Kati Ya Polisi Na Baadhi Ya Wafuasi Wake Waliokuwa Wakipinga Kukamatwa Huko. Baadaye Alisafirishwa Kwa Ndege Hadi Hapa Nairobi Alipowasilishwa Kwa Tume Ya Maadili Na Kupambana Na Ufisadi EACC. Sonko Anakabiliwa Na Tuhuma Za Kujipatia Mali Na Pesa Kwa Njia Isiyo Halali Miongoni Mwa Mashtaka Mengine Ya Kuhujumu Uchumi.