4th December, 2019
Awamu ya pili ya maonyesho yatakayodumu juma zima na ambayo yanawaleta pamoja vijana wa Pwani na uvumbuzi wao yameanza hii leo katika Kaunti ya Mombasa. Wageni mbalimbali wa kimataifa akiwemo balozi wa Uingereza watahudhuria katika hafla hii yenye madhumuni ya kukuza talanta katika sekta ya teknolojia na mawasiliano miongoni mwa vijana.