4th December, 2019
Margaret Nyakango ndiye msimamizi mpya wa bajeti za serikali. Nyakango ameapishwa kwenye sherehe iliyoongozwa na jaji mkuu David Maraga katika mahakama ya upeo hapa Nairobi. Nyakango aliyeteuliwa na rais Uhuru Kenyatta mwezi jana anamrithi Agnes Odhiambo. Nyakango ni mhasibu na atahudumu kama msimamizi wa bajeti kwa muda wa miaka minane.