4th December, 2019
Mahakama kuu imesitisha ada ya shilingi mia nne ya maegesho ya magari, ambayo serikali ya kaunti ya nairobi ilikuwa imepitisha kuwa itaanza kutekelezwa hii leo. Hii ni baada ya shirikisho la matumizi ya huduma na bidhaa ( COFEK) kuwasilisha kesi ya kupinga ada hiyo kupandishwa maradufu kutoka shilingi 200 hadi shilingi 400.