18th November, 2019
Mamia Ya Wakazi Wa Kaunti Ya Tanariver Walifanya Maandamano Mjini Hola Jumamosi Iliyopita Wakiilalamikia Hatua Ya Serikali Kukosa Kumtia Mbaroni Gavana Wa Garissa Ali Korane, Naibu Wake Sawa Na Mbunge Wa Fafi Kwa Madai Ya Kuchochea Uhasama Baina Ya Jamii Zinaoshi Kwenye Mpaka Wa Kaunti Hizo Mbili. Wakibeba Mabango Na Kuimba Nyimbo Za Kutaka Haki Wakazi Hao Walifululiza Hadi Hola Mjini Kutoka Uwanja Wa Bayusuf Na Kuelekea Kwenye Afisi Za Kamishna Wa Kaunti, Na Gavana Wakisistiza Kutiwa Mbaroni Kwa Watatu Hao.