15th November, 2019
Huenda Baadhi Ya Mawaziri Wa Kaunti Ya Mombasa Wakatemwa Baada Ya Muhula Wao Wakuhudumu Kutamatika Usiku Wa Jumanne.Haya Ni Kwa Mujibu Wa Gavana Wa Mombasa Ali Hassan Joho. Katika Mahojiano Ya Kipekee Na Mwanahabari Wetu Tobias Chanji, Joho Amesema Kuwa Mawaziri Tisa Kwa Sasa Hawana Ajira Na Kwamba Wanaendelea Kupigwa Msasa Utendakazi Wao Na Jopo Maalum.Jopo Hili Linatarajiwa Kutoa Ripoti Yake Siku Tatu Zijazo Na Kubaini Mawaziri Wapi Watakaofurushwa Na Wale Watakaosalia.