12th November, 2019
Chama Cha Odm Kitajipata Tena Kwenye Majaribio Ya Ubabe Wa Kisiasa Huko Kilifi Baada Ya Mwakilishi Wadi Ya Dabaso Emmanuel Changawa Kupotez Akiti Chake. Spika Wa Kaunti Ya Kilifi Jimmy Kahindi Alitangaza Kuwa Kiti Hicho Kiko Wazi Hapo Jana. Hii Ni Baada Ya Kesi Iliyowasilishwa Mahakamani Na Dickson Kalama Kupinga Uchaguzi Huo. Sasa Tume Ya Uchaguzi Ina Hadi Siku Tisini Kuitangaza Siku Ya Uchaguzi Mdopgo Wa Dabaso. Itakumbukwa Kuwa Mwezi Oktoba Odm Ilitanuana Misuli Na Muasi Wao Bi Aisha Jumwa Aliyekuwa Akimuunga Mkono Mgombeaji Huru Abdirahman Omar Katika Uchaguzi Mdogo Wa Ganda Kaunti Hiyo Ya Kilifi.Reuben Katana Wa Odm Alishinda Kiti Hicho Ambapo Mtu Mmoja Alipigwa Risasi Na Kufariki Katika Vurumai Za Mkesha Wa Kura. Vilevile Wiki Jana Odm Ilishinda Uchaguzi Mdogo Wa Ubunge Huko Kibra Ulioashiria Uhasama Wakisiasa Baina Ya Raila Odinga Na Naibu Rasi William Ruto